
Kutatua Hatia ya Utoaji Mimba
30 June 2026Wajibu wa Tumaini katika Maisha ya Kikristo
Mambo matatu ya maadili ya Kikristo yanayotegemeana—imani, tumaini, na upendo—yote ni muhimu. Kama vile upendo ulivyo muhimu (1 Wakorintho 13:13), tunajua kwamba imani si kuwa haina muhimu. Tumekuwa tukifanya kazi kwa karibu juu ya umuhimu wa imani, na tunaelewa umuhimu wa upendo, lakini mara nyingi kipengele cha tatu kati ya maadili haya matatu yanayo tegemeana katika utatu huu wa maadili, tumaini, inapuuzwa katika tajiriba ya Kikristo.
Ikiwa kuna neno lolote katika Warumi 5 ambalo tunaweza kulielewa vibaya kabisa, ni tumaini. Daima kuna kipengele fulani cha shaka kinachotia ukungu uelewa wetu kuhusu matumizi ya Paulo ya neno hilo. Tunapotumia neno tumaini, kwa kawaida tunalitumia kuelezea matamanio au shauku kwamba jambo fulani litatokea, jambo ambalo hatuna uhakika kama kweli litatokea. Hivyo sivyo jinsi neno hilo linavyofanya kazi katika Agano Jipya. Tunapofanywa upya na Roho Mtakatifu, tunazaliwa upya kwa tumaini ambalo linaunda msingi wa ujasiri wetu katika kuishi maisha ya Kikristo. Tofauti pekee kati ya tumaini na imani ni kwamba imani inaangalia kile ambacho tayari kimefanyika, nasi tunaweka tumaini letu ndani yake. Tumaini ni imani inayoangalia mbele.
Sitiari iliyotumika katika Agano Jipya kuelezea asili ya tumaini ni ile ya nanga. Tunaambiwa kuwa tumaini ni nanga ya roho. Mara nyingi tunakutana na taswira hii ya baharini katika Agano Jipya. Wale ambao si imara wanalinganishwa na mashua zisizo na nanga, zinazorushwa huku na huko na kila upepo wa mafundisho. Watu wa aina hiyo wana sifa ya kusitasita na kutokuwa na uhakika, lakini tumaini lililopandwa katika roho na Roho Mtakatifu si kama hilo. Tumaini hili linatoa msingi na uthabiti na uhakika. Tumaini ni nanga inayotuzuia tusipeperushwe. Ni matumaini kwamba hakika Mungu atafanya kila kitu ambacho amesema atafanya.
Tunda la kuhesabiwa haki ni la aina hiyo ya tumaini. Kuhesabiwa haki, kwa namna fulani, ni malipo ya awali kwa yote ambayo Mungu anatuhahidi katika kazi yake ya ukombozi. Tumaini huumbwa na Roho Mtakatifu ndani yetu. Mahali pengine Paulo atazungumza kuhusu Mungu kutupa “dhamana” au malipo ya awali ya Roho Mtakatifu, ambayo hutupa uhakika kamili kwa ajili ya siku zijazo. Matumaini siyo kuvuta pumzi ndefu na kutumaini kwamba mambo yatakuwa sawa. Ni uhakika kwamba Mungu atafanya kile Anachosema Atakifanya.
Makala haya yalichapishwa awali kwenye Blogu ya Ligonier Ministries.


