Jinsi ya Kusoma Fasihi ya Hekima
12 February 2026
Jinsi ya Kukumbuka na Kutenda Biblia
19 February 2026
Jinsi ya Kusoma Fasihi ya Hekima
12 February 2026
Jinsi ya Kukumbuka na Kutenda Biblia
19 February 2026

Jinsi ya Kusoma Manabii

Manabii ni vigumu kuwaelewa. Kwa sehemu, hiyo ni kwa sababu Mungu alijifunua kwao katika ndoto na maono. Ni kwa Musa pekee Mungu alizungumza ana kwa ana (Hesabu 12:6–8). Manabii Wakuu ni pamoja na Isaya, Yeremia, Ezekieli, na Danieli. Manabii Wadogo ni pamoja na Hosea, Yoeli, Amosi, Obadia, Yona, Mika, Nahumu, Habakuki, Sefania, Hagai, Zekaria, na Malaki. Hapa kuna vidokezo kadhaa vitakavyokusaidia kusoma na kuelewa Vitabu vya Unabii.

1. Chunguza muktadha.

Kwanza, elewa kadiri uwezavyo kuhusu tukio la kihistoria, mazingira ya kijamii, na nabii unayemsoma. Biblia nzuri ya kujifunza, kama vile Biblia ya Kujifunza ya Mabadiliko, inaweza kusaidia katika hili.

2. Tambua jukumu la manabii kama wanasheria wa agano la Mungu.

Pili, tambua kwamba manabii kimsingi walikuwa wanasheria wa agano la Mungu. Ingawa walizungumza kuhusu sehemu nyingi za agano—kwa mfano, dibaji na utangulizi wa kihistoria (“Mimi ni Bwana Mungu wako niliyekutoa katika nchi ya Misri”), na mara nyingi waliwakumbusha watu wajibu wao wa kutimiza amri za Mungu (yaani, “masharti”)—kusudi lao kuu lilikuwa kuwasilisha vikwazo vya agano. Katika lugha ya kawaida leo, tunatabia ya kuona vikwazo kuwa hasi tu (kwa mfano, “vikwazo vya kiuchumi”). Lakini katika Maandiko, vikwazo vinaweza kuwa chanya au hasi. Kwa maneno mengine, baraka kwa utiifu, na laana au adhabu kwa kutotii. Kama wanasheria wazuri, manabii walikusanya mashtaka yao dhidi ya mfalme na/au watu na kuwahubiria kuhusu jinsi walivyoshindwa kuishi kulingana na viwango vya Mungu.

3. Jifunze kuwa na ufahamu wa lugha ya kinabii.

Lugha ya kinabii ni kipengele muhimu cha jinsi Manabii wanavyoongea kuhusu hali za baadaye. Hapa, dhana kuu ni kwamba Manabii, ambao mara kwa mara huzungumzia utunzaji na mipango ya Israeli na makabila, ardhi yao, na hekalu lao, mara nyingi sana wanaelezea hali mpya za agano ambazo bado hazijafika. Kwa hiyo, msomaji anapaswa kujiuliza  maswali haya mara kwa mara, “Je, mambo ya kisasa yanayomzunguka nabii, ndiyo anayozungumzia kweli? Au, anazungumzia hali za baadaye?” Lugha ya kinabii, kwa hiyo, ni namna ya maelezo ambayo manabii wa Agano la Kale hutumia mpangilio wa vielelezo vya mambo ya Israeli ili kuonyesha hali za Kimasihi za enzi ya agano jipya. Hii ndiyo asili ya lugha ya kinabii, na kama hatuitambui, basi tutawaelewa Manabii vibaya.

Hili ndilo Paulo alilolijua vizuri, hata katika rufaa yake mbele ya Agripa (Matendo 26:19–29). Paulo anawasihi manabii, kwamba wanazungumzia Kristo na utume wa Paulo kwa watu wa mataifa. Lugha ya manabii, aina ya lugha ya kielelezo wanayotumia kujieleza, inahitaji (hasa kwa muumini wa agano jipya) kutenganisha lugha ya nje na uhalisia wa ahadi za agano jipya.

Kwa kifupi, katika lugha ya kinabii, manabii mara nyingi wanaelezea agano jipya kwa kutumia hali za taasisi za agano la kale. Lugha ya unabii, taswira wanayotumia manabii, na misemo wanayotumia katika maelezo yao, mara nyingi hutumika kuonyesha kile kitakachotokea katika Kristo Yesu na kwa wanadamu wote. Hili linakuwa muhimu, kwa mfano, katika maelezo ya uhamisho na kutawanyika, kukusanywa kwa makabila, kurudi katika nchi, na namna ya laana. Ingawa manabii hawazungumzi kwa ujuzi wote kuhusu siku zijazo, mara nyingi huzungumzia uhakika wa kuja kwa Mungu katika Yesu Kristo, agano jipya, na hata ujio wa pili wa Bwana wetu, bila kutofautisha sehemu zote kutoka kwa nyingine. Hata hivyo, bado kuna umoja wa kimsingi katika hatua mbalimbali wanazozungumzia chini ya uvuvio wa Roho Mtakatifu.

Kwa mfano, wakati Yoeli anapozungumzia kuhusu kumiminwa kwa Roho na picha za siku kuu na ya kutisha ya kuja kwa Bwana, hakuwa akizungumza tu na wasikilizaji wake wa awali (Yoeli 2:28–32). Yoeli 2 imenukuliwa katika Matendo ya Mitume wakati wa Pentekote (Matendo 2:17–21). Picha zile zile zilizoonyeshwa katika Matendo 2:28–32 pia zinaonekana wakati wa kusulubiwa kwa Kristo. Mtu anaweza hata kusema kwa uhalali kwamba unabii wa Yoeli hatimaye unatimia katika kuja kwa pili kwa Bwana wetu. Kwa hiyo, ingawa Yoeli alikuwa na nia moja, maneno yake yanapata marejeleo mengi (yaani, “sehemu za kutua”) katika historia ya ukombozi. Ndiyo maana kifungu hiki kuhusu kumiminwa kwa Roho kilikuwa mojawapo ya vifungu vilivyopendwa na John Calvin katika kuelezea jinsi lugha ya kinabii inavyofanya kazi.

4. Tafuta njia ambazo Maandiko ya Agano Jipya yanavyo nukuu, kuashiria, au kuiga Manabii.

Nne, na hatimaye, kwa kuwa Kristo aliwaambia wanafunzi wake njiani kuelekea Emau kwamba Maandiko yote yalizungumza juu Yake na huduma Yake (au kwa upanuzi mwili Wake, ambao ni kanisa), tunapaswa daima kuwa katika harakati za kutafuta njia ambazo Maandiko ya Agano Jipya yanataja, yanarejelea, au yanarudia Manabii. Kwa mfano, Petro (akiwa shahidi wa kubadilika kwa sura) alitambua kwamba kifungu cha msingi katika Kumbukumbu la Torati 18:15–19, ambacho kinazungumza juu ya Musa kama nabii wa mfano wa manabii wote waliokuja baadaye, kilipata utimilifu wake wa mwisho katika Kristo kama nabii wa mwisho (angalia Matendo 3:17–26). Fasiri hii inathibitishwa zaidi na mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye alielewa kwamba Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi juu ya nyumba Yake (agano la kale) lakini Kristo ni mwaminifu kama mwana juu ya nyumba Yake; yaani, agano jipya. Zaidi ya hayo, Mungu ndiye mjenzi wa nyumba nzima, ya kale na mpya (Ebr. 3:1–6).

Makala hii ni sehemu ya mkusanyiko wa Hemenitiki (taaluma ya ufasiri wa Biblia).

Bryan D. Estelle
Bryan D. Estelle
Dr. Bryan D. Estelle is professor of Old Testament at Westminster Seminary California in Escondido, California. He is author of Echoes of Exodus.