Jinsi ya Kusoma Fasihi ya Ufunuo
5 March 2026
Jinsi ya Kusoma Fasihi ya Ufunuo
5 March 2026

Ufafanuzi wa Maandiko ni Nini?

Katika siku zetu, mara nyingi tunasikia kwamba hakuna maoni ya mtu yanapaswa kuwa na upendeleo juu ya maoni ya mwingine, kwamba hakuna mtu aliye na haki ya pekee juu ya ukweli, na kwamba kila kitu hatimaye ni suala la maoni. Mtazamo huu unatumika hata katika Maandiko, kufikia mahali ambapo maana ya Biblia inaonekana kuwa rahisi na inayobadilika bila kikomo. Mafundisho ya Mageuzo yamekataa maoni haya kila mara, kwa sababu rahisi kwamba Maandiko ni Neno la Mungu, na Mungu anajali jinsi Neno lake linavyosomwa. Hatimaye, Maandiko lazima yasomwe jinsi Mungu anavyoelekeza.

Kufafanua na kuelewa maandiko ya Biblia ni kipaji cha Ufafanuzi wa maandiko kwa usahihi kulingana na muktadha wake wa asili. Ufafanuzi wa maandiko kwa usahihi kulingana na muktadha wake wa asili unahusiana kwa karibu na ufafanuzi wa maandiko kwa kutumia kanuni sahihi, ambao unahusisha kanuni kulingana na ambavyo Maandiko yanashughulikiwa na kufafanuliwa. Kwa hivyo, ni matumizi ya ufafanuzi wa Maandiko kwa kutumia kanuni sahihi katika kifungu fulani. Hapa kuna baadhi ya kanuni za kufafanua Biblia kulingana na mafundisho ya mageuzo.

Tunapaswa kuifafanua Biblia kwa unyenyekevu.

Biblia si kitabu cha kawaida. Ni kitabu cha kipekee, Neno halisi la Mungu, kanuni pekee isiyoweza kukosea ya imani na utendaji, na kwa hiyo tunapokisoma, tunajaribu kutambua kile ambacho Mungu aliye hai anatuambia. Mamlaka nyingine zote—hata zile zinazokusudia kutuambia jinsi ya kufafanua Maandiko—ziko chini ya Maandiko. Hivyo, ingawa tunatafuta kutambua maana iliyokusudiwa na waandishi wa kibinadamu, hatimaye tunatafuta kutambua maana iliyokusudiwa na Mwandishi huyo wa Kiungu.

Hii ina maana ya kujiweka chini ya Biblia badala ya juu yake. Tunapofikia kifungu ambacho maana yake dhahiri tunaona kuwa ya kuchukiza, kwa mfano, hatujaribu kukifafanua visivyo au kukipuuza. Kwa mfano, katika Yohana 6, Yesu anazungumza juu ya kipaumbele cha neema ya Mungu ya kuchagua katika kuleta imani kwa wale wanaomtumaini. Wengi huona fundisho hilo kuwa gumu sana na hulpuuza(Yohana 6:66), na wengi leo vile vile hujaribu kueleza visivyo mafundisho ya Maandiko juu ya uchaguzi. Hata hivyo ni lazima tujitahidi kuelewa na kutii mafundisho ya Maandiko kama yalivyo na si kama vile tungependa yawe.

Tunapaswa kufafanua Biblia kwa uaminifu.

Kufafanua Biblia kwa uaminifu kunamaanisha kusoma kifungu fulani kama kilivyokusudiwa kusomwa. Kusoma kwa njia hii hutilia maanani vitu kama vile aina na tamathali za usemi na huzingatia muktadha wa kihistoria na kifasihi wa kifungu fulani, huku ukizingatia jinsi maneno yaliyotumiwa yalivyoeleweka wakati maandishi yalipoandikwa. Mbinu hii mara nyingi huitwa ufafanuzi wa kihistoria-kisarufi, na inakusudiwa kufichua kile ambacho mwandishi alikusudia kuwasilisha kwa kuzingatia maneno aliyotumia na maana yake katika muktadha.

Kusoma Biblia kwa uaminifu huanza kwa kuuliza baadhi ya maswali muhimu kuhusu kile kifungu, ikiwa ni pamoja na: Mwandishi ni nani? Muktadha wa uandishi wake ulikuwa ni nini? Kusudi lake la kuandika lilikuwa ni nini? Ni aina gani ya maandishi? Majibu ya maswali haya mara nyingi yanaweza kupatikana katika maandishi yenyewe, lakini wakati mwingine nyenzo za nje kama vile tahariri na kamusi za Biblia zinaweza kusaidia.

Maneno kwa kawaida huwa na maana au viashiria zaidi ya kimoja, na muktadha hutusaidia kuamua ni maana gani hasa ya neno inayokusudiwa kati ya maana zake zote zinazowezekana—katika uwiano wake wa kisemantiki (ona, kwa mfano, njia mbalimbali ambazo neno “ulimwengu” limetumika katika Agano Jipya: Mt. 4:8; 13:22; 25:34; Mk 4:19; Lk 2:1; Yoh 3:7; Yoh 3:1:2. 3:6; Maneno muhimu kama vile kwa hiyo, badala yake, lakini,* badala yake*, na hivyo huonyesha mtiririko wa mawazo ya mwandishi, na sarufi ya kifungu inaweza kuonyesha msisitizo (kwa mfano, Luka 12:5).

Kubainisha aina ya kifungu kunaweza pia kutusaidia kutambua kile mwandishi anachokusudia. Biblia ina sehemu za mashairi, unabii, fasihi ya ufunuo, maagizo, na kadhalika, kila moja ikiwa na kanuni zake zinazoeleza jinsi andiko linavyopaswa kueleweka. Kwa mfano, ikiwa kifungu ni shairi, huenda kuna vielelezo na taswira zinazoelekeza kwenye maana zaidi ya iliyo halisi. Ni vivyo hivyo kwa ufunuo. Ikiwa ni simulizi, inaweza kumaanisha tu kuhusisha mfululizo wa matukio, lakini matukio hayo yanaweza kuwa kielelezo cha matukio ya baadaye au kuwa na umuhimu mkubwa katika historia ya ukombozi.

Kuchunguza vipengele hivi vya maandishi kunaweza kutueleza maana yake wakati yalipoandikwa. Kuanzia hapo, tunaweza kujaribu kuelewa kile kifungu kinamaanisha nini kwetu sasa. Utaratibu huu unahusisha kuamua maana ya kifungu katika mwanga wa ujio wa Kristo. Sasa kwa kuwa Kristo amekuja, tunapaswa kuelewaje amri hii au kuisoma simulizi hili? Je, sisi, kama washiriki wa kanisa la Agano Jipya, tunapaswa kuona ahadi ya kuamini, amri ya kutii, onyo la kutii, ukweli wa kuelewa, au dawa ya kutumia?

Tunapaswa kutafsiri Biblia kwa kuwajibika.

Kwa sababu Mungu ndiye Mwandishi mkuu wa Maandiko, Yeye hutoa ufafanuzi wa uhakika. Hii ina maana kwamba Maandiko hufafanua Maandiko. Ungamo la Imani la Westminster linasema, “Kanuni isiyoweza kukosea ya kufafanua Maandiko ni Maandiko yenyewe: na kwa hiyo, kunapokuwa na swali kuhusu maana ya kweli na kamili ya Maandiko yoyote (ambayo si mengi, lakini moja), ni lazima yachunguzwe na kujulikana kwa sehemu nyingine zinazozungumza kwa uwazi zaidi” (1.9). Ni lazima mara nyingi tutazame mahali pengine katika Biblia ili kutoa nuru juu ya vifungu vyenye matatizo. Ufafanuzi wa uhakika wa Maandiko unapatikana ndani ya Maandiko, si katika rufaa kwa mamlaka nyingine kama vile mapokeo, viongozi wa kanisa, au maoni.

Ungamo la Westminster pia linasema kwamba “katika matumizi yafaayo ya njia za kawaida” ujumbe wa Maandiko unaweza kufichuliwa (1.7). Maandiko yanapaswa kusomwa kwa njia ya kawaida, kama kitabu kingine chochote, kwa kutumia kanuni za kawaida za sarufi na kadhalika, na haipaswi kuwa tu mahali pa kuzindua kwa uvumi, tafsiri ya mfano, na dhana zinazopuruka. Pia yapasa kusomwa kwa uzito—kwa “matumizi ya kawaida yanayostahili.” Mtu hawezi kuichukulia Biblia kipuuzi na kisha kutamka kuwa haieleweki.

Hatimaye, tunataka kujua Biblia inatuambia nini kuhusu Mungu ni nani na ametufanyia nini katika Kristo. Kila kifungu kimejaa maana inayoweza kutumika katika maisha yetu, lakini ni muhimu tuone jinsi matumizi haya yanavyotiririka kutoka kwa muungano wetu na Kristo kupitia imani. Hatujaahidiwa maisha yenye mafanikio bila masharti. Kwa mfano, katika Yeremia 29:11, Mungu hapo awali aliweka tumaini la baraka kwa Waisraeli waliokuwa uhamishoni Babeli. Lakini Kristo, kama Mwana mtiifu kabisa na  Israeli wa kweli, alirithi ahadi zote za Mungu na kustahili thawabu zote za Mungu, na kwa sababu ya muungano wetu naye, tunapokea baraka zisizohesabika (Efe. 1:3–11). Hii ni habari njema, na inafunuliwa katika kila ukurasa wa Maandiko.


Makala hii ni sehemu ya mkusanyiko wa Hemenitiki (taaluma ya ufasiri wa Biblia).

Kevin D. Gardner
Kevin D. Gardner
Kevin D. Gardner is associate editor of Tabletalk magazine, resident adjunct professor at Reformation Bible College in Sanford, Fla., and a teaching elder in the Presbyterian Church in America.
Jinsi ya Kusoma Fasihi ya Ufunuo
5 March 2026
Ufafanuzi wa Maandiko ni Nini?
10 March 2026

Katika siku zetu, mara nyingi tunasikia kwamba hakuna maoni ya mtu yanapaswa kuwa na upendeleo juu ya maoni ya mwingine, kwamba hakuna mtu aliye na haki ya pekee juu ya ukweli, na kwamba kila kitu hatimaye ni suala la maoni. Mtazamo huu unatumika hata katika Maandiko, kufikia mahali ambapo maana ya Biblia inaonekana kuwa rahisi na inayobadilika bila kikomo. Mafundisho ya Mageuzo yamekataa maoni haya kila mara, kwa sababu rahisi kwamba Maandiko ni Neno la Mungu, na Mungu anajali jinsi Neno lake linavyosomwa. Hatimaye, Maandiko lazima yasomwe jinsi Mungu anavyoelekeza.

Kufafanua na kuelewa maandiko ya Biblia ni kipaji cha Ufafanuzi wa maandiko kwa usahihi kulingana na muktadha wake wa asili. Ufafanuzi wa maandiko kwa usahihi kulingana na muktadha wake wa asili unahusiana kwa karibu na ufafanuzi wa maandiko kwa kutumia kanuni sahihi, ambao unahusisha kanuni kulingana na ambavyo Maandiko yanashughulikiwa na kufafanuliwa. Kwa hivyo, ni matumizi ya ufafanuzi wa Maandiko kwa kutumia kanuni sahihi katika kifungu fulani. Hapa kuna baadhi ya kanuni za kufafanua Biblia kulingana na mafundisho ya mageuzo.

Tunapaswa kuifafanua Biblia kwa unyenyekevu.

Biblia si kitabu cha kawaida. Ni kitabu cha kipekee, Neno halisi la Mungu, kanuni pekee isiyoweza kukosea ya imani na utendaji, na kwa hiyo tunapokisoma, tunajaribu kutambua kile ambacho Mungu aliye hai anatuambia. Mamlaka nyingine zote—hata zile zinazokusudia kutuambia jinsi ya kufafanua Maandiko—ziko chini ya Maandiko. Hivyo, ingawa tunatafuta kutambua maana iliyokusudiwa na waandishi wa kibinadamu, hatimaye tunatafuta kutambua maana iliyokusudiwa na Mwandishi huyo wa Kiungu.

Hii ina maana ya kujiweka chini ya Biblia badala ya juu yake. Tunapofikia kifungu ambacho maana yake dhahiri tunaona kuwa ya kuchukiza, kwa mfano, hatujaribu kukifafanua visivyo au kukipuuza. Kwa mfano, katika Yohana 6, Yesu anazungumza juu ya kipaumbele cha neema ya Mungu ya kuchagua katika kuleta imani kwa wale wanaomtumaini. Wengi huona fundisho hilo kuwa gumu sana na hulpuuza(Yohana 6:66), na wengi leo vile vile hujaribu kueleza visivyo mafundisho ya Maandiko juu ya uchaguzi. Hata hivyo ni lazima tujitahidi kuelewa na kutii mafundisho ya Maandiko kama yalivyo na si kama vile tungependa yawe.

Tunapaswa kufafanua Biblia kwa uaminifu.

Kufafanua Biblia kwa uaminifu kunamaanisha kusoma kifungu fulani kama kilivyokusudiwa kusomwa. Kusoma kwa njia hii hutilia maanani vitu kama vile aina na tamathali za usemi na huzingatia muktadha wa kihistoria na kifasihi wa kifungu fulani, huku ukizingatia jinsi maneno yaliyotumiwa yalivyoeleweka wakati maandishi yalipoandikwa. Mbinu hii mara nyingi huitwa ufafanuzi wa kihistoria-kisarufi, na inakusudiwa kufichua kile ambacho mwandishi alikusudia kuwasilisha kwa kuzingatia maneno aliyotumia na maana yake katika muktadha.

Kusoma Biblia kwa uaminifu huanza kwa kuuliza baadhi ya maswali muhimu kuhusu kile kifungu, ikiwa ni pamoja na: Mwandishi ni nani? Muktadha wa uandishi wake ulikuwa ni nini? Kusudi lake la kuandika lilikuwa ni nini? Ni aina gani ya maandishi? Majibu ya maswali haya mara nyingi yanaweza kupatikana katika maandishi yenyewe, lakini wakati mwingine nyenzo za nje kama vile tahariri na kamusi za Biblia zinaweza kusaidia.

Maneno kwa kawaida huwa na maana au viashiria zaidi ya kimoja, na muktadha hutusaidia kuamua ni maana gani hasa ya neno inayokusudiwa kati ya maana zake zote zinazowezekana—katika uwiano wake wa kisemantiki (ona, kwa mfano, njia mbalimbali ambazo neno “ulimwengu” limetumika katika Agano Jipya: Mt. 4:8; 13:22; 25:34; Mk 4:19; Lk 2:1; Yoh 3:7; Yoh 3:1:2. 3:6; Maneno muhimu kama vile kwa hiyo, badala yake, lakini,* badala yake*, na hivyo huonyesha mtiririko wa mawazo ya mwandishi, na sarufi ya kifungu inaweza kuonyesha msisitizo (kwa mfano, Luka 12:5).

Kubainisha aina ya kifungu kunaweza pia kutusaidia kutambua kile mwandishi anachokusudia. Biblia ina sehemu za mashairi, unabii, fasihi ya ufunuo, maagizo, na kadhalika, kila moja ikiwa na kanuni zake zinazoeleza jinsi andiko linavyopaswa kueleweka. Kwa mfano, ikiwa kifungu ni shairi, huenda kuna vielelezo na taswira zinazoelekeza kwenye maana zaidi ya iliyo halisi. Ni vivyo hivyo kwa ufunuo. Ikiwa ni simulizi, inaweza kumaanisha tu kuhusisha mfululizo wa matukio, lakini matukio hayo yanaweza kuwa kielelezo cha matukio ya baadaye au kuwa na umuhimu mkubwa katika historia ya ukombozi.

Kuchunguza vipengele hivi vya maandishi kunaweza kutueleza maana yake wakati yalipoandikwa. Kuanzia hapo, tunaweza kujaribu kuelewa kile kifungu kinamaanisha nini kwetu sasa. Utaratibu huu unahusisha kuamua maana ya kifungu katika mwanga wa ujio wa Kristo. Sasa kwa kuwa Kristo amekuja, tunapaswa kuelewaje amri hii au kuisoma simulizi hili? Je, sisi, kama washiriki wa kanisa la Agano Jipya, tunapaswa kuona ahadi ya kuamini, amri ya kutii, onyo la kutii, ukweli wa kuelewa, au dawa ya kutumia?

Tunapaswa kutafsiri Biblia kwa kuwajibika.

Kwa sababu Mungu ndiye Mwandishi mkuu wa Maandiko, Yeye hutoa ufafanuzi wa uhakika. Hii ina maana kwamba Maandiko hufafanua Maandiko. Ungamo la Imani la Westminster linasema, “Kanuni isiyoweza kukosea ya kufafanua Maandiko ni Maandiko yenyewe: na kwa hiyo, kunapokuwa na swali kuhusu maana ya kweli na kamili ya Maandiko yoyote (ambayo si mengi, lakini moja), ni lazima yachunguzwe na kujulikana kwa sehemu nyingine zinazozungumza kwa uwazi zaidi” (1.9). Ni lazima mara nyingi tutazame mahali pengine katika Biblia ili kutoa nuru juu ya vifungu vyenye matatizo. Ufafanuzi wa uhakika wa Maandiko unapatikana ndani ya Maandiko, si katika rufaa kwa mamlaka nyingine kama vile mapokeo, viongozi wa kanisa, au maoni.

Ungamo la Westminster pia linasema kwamba “katika matumizi yafaayo ya njia za kawaida” ujumbe wa Maandiko unaweza kufichuliwa (1.7). Maandiko yanapaswa kusomwa kwa njia ya kawaida, kama kitabu kingine chochote, kwa kutumia kanuni za kawaida za sarufi na kadhalika, na haipaswi kuwa tu mahali pa kuzindua kwa uvumi, tafsiri ya mfano, na dhana zinazopuruka. Pia yapasa kusomwa kwa uzito—kwa “matumizi ya kawaida yanayostahili.” Mtu hawezi kuichukulia Biblia kipuuzi na kisha kutamka kuwa haieleweki.

Hatimaye, tunataka kujua Biblia inatuambia nini kuhusu Mungu ni nani na ametufanyia nini katika Kristo. Kila kifungu kimejaa maana inayoweza kutumika katika maisha yetu, lakini ni muhimu tuone jinsi matumizi haya yanavyotiririka kutoka kwa muungano wetu na Kristo kupitia imani. Hatujaahidiwa maisha yenye mafanikio bila masharti. Kwa mfano, katika Yeremia 29:11, Mungu hapo awali aliweka tumaini la baraka kwa Waisraeli waliokuwa uhamishoni Babeli. Lakini Kristo, kama Mwana mtiifu kabisa na  Israeli wa kweli, alirithi ahadi zote za Mungu na kustahili thawabu zote za Mungu, na kwa sababu ya muungano wetu naye, tunapokea baraka zisizohesabika (Efe. 1:3–11). Hii ni habari njema, na inafunuliwa katika kila ukurasa wa Maandiko.


Makala hii ni sehemu ya mkusanyiko wa Hemenitiki (taaluma ya ufasiri wa Biblia).